Posts

Diego Costa apewa muda zaidi kupumzika Chelsea

Image
  Costa alifungia Chelsea mechi yao ya mwisho, fainali Kombe la FA walipolazwa na Arsenal    Mshambuliaji Diego Costa amepewa muda zaidi wa kumpumzika na Chelsea, hatua iliyozidisha uwezekano kwamba huenda akaihama klabu hiyo majira haya ya joto. Mhispania huyo wa miaka 28 amehusishwa na kuhaam klabu hiyo baada ya kufahamishwa na meneja Antonio Conte kwamba hayupo kwenye mipango yake. Costa hakujiunga na wenzake kwa mazoezi Jumatatu. "Iliafikiwa kati yake na klabu kwamba anafaa kuchukua siku zaidi kupumzika," taarifa kwenye klabu hiyo ilisema. Costa anatarajiwa kutohudhuria mazoezi wiki hii. Mshambuliaji huyo alikuwa mchezaji pekee ambaye hakufika uwanja wa mazoezi wa Chelsea Cobham kando na Antonio Rudiger, ambaye alijiunga na klabu hiyo Jumapili. Costa aliwajulisha wanahabari kwamba Conte alikuwa amemwandikia ujumbe wa simu kwamba hakuwa kwenye mipango yake mwezi jana, na inaarifiwa kwamba msimamo wake haujabadilika. Du

Mwanamke aikojolea bendera ya Marekani

Image
    Emily Lance alitengeza video akiikojolea bendera ya Marekani Mwanamke aliyesambaza kanda yake ya video akiikojolea bendera ya Marekani ametoa wito kwa watu kutoilenga familia yake akisema hawaungi mkono tendo lake. Emily Lance alipokea vitisho vya mauaji katika mtandao wa kijamii na ubakaji baada ya kuchapisha kanda hiyo ya video siku ya uhuru wa taifa hilo. Akaunti yake haiko tena katika mtandao wake wa facebook lakini awali alikuwa amechapisha kwamba babake na eneo analofanya kazi pia limelengwa, kulingana na ripoti. Kutoheshimu bendera ya Marekani sio kinyume cha sheria kutokana na sheria nyingi na uhuru wa kujieleza. Katika kanda hiyo ya video, Bi Lance anaonekana akisimama juu ya choo ambapo bendera ya Marekani imewekwa na kuikojolea kupitia usaidizi wa chombo ambacho kinawasaidai wanawake kufanya hivyo wakiwa wamesimama. Chini yake aliandika maneneo ya kuitusi bendera hiyo. Baadaye aliwataka wanaopinga wazo lake kutowalenga watu wasio na

Boni: Kenya yaanza kuangusha mabomu ‘msitu wa al-Shabab’

Image
    Bw Marwa (kati) amewataka raia kutii amri ya kuuhama msitu huo  Kenya imetangaza kwamba imeanza kutekeleza mashambulio ya kutoka angani katika msitu wa Boni karibu na mpaka wa nchi hiyo na Somalia. Wenyeji wanaoishi msituni wanahamishwa hadi kwenye kambi zilizotengwa na serikali kabla ya mabomu kurushwa. Wanamgambo wa al-Shabaab wanadaiwa kugeuza msitu huo kuwa makao na ngome yao. Wanamgambo hao wanadaiwa kutumia msitu huo kutekeleza mashambulio katika maeneo ya karibu. Wiki iliyopita, watu 9 waliuawa kwa kukatwa shingo na wapiganaji hao katika kijiji cha Pandanguo kilicho karibu na msitu huo katika kaunti ya Lamu. Jumamosi, serikali ilirejesha tena amri ya kutotoka nje usiku katika maeneo ya pwani na kaskazini mashariki mwa Kenya ambayo yameshuhudia mashambulio ya kigaidi kutoka kwa al-Shabab. Mwandishi wa BBC Ferdinand Omondi anasema wanajeshi wa Kenya wamejaribu kuwafurusha wanamgambo hao kutoka msitu wa Boni kwa miaka miwili bila mafanikio. Kamishna wa k

Antonio Rudiger: Chelsea wamnunua beki kutoka Ujerumani

Image
  Antonio Rudiger alisaidia Ujerumani kushinda Kombe la Mabara mwaka 2017 nchini Urusi  Mabingwa wa Ligi Kuu ya England Chelsea wamemnunua beki Mjerumani Antonio Rudiger kutoka klabu ya AS Roma kwa mkataba wa miaka mitano kwa £29m. Rudiger, 24, alikamilisha uhamisho wake wiki moja baada ya kusaidia mabingwa wa dunia Ujerumani kushinda Kombe la Mabara. "Ni jambo linalonifurahisha sana kwa sababu si kila mchezaji anayepata fursa ya kujiunga na klabu kubwa kama hii," alisema Rudiger. Ada waliyolipa Chelsea inaweza ikapanda na kufikia £33.3m ukiongeza vikolezo vilivyo kwenye mkataba wake. "Antonio bado ana umri mdogo lakini ana uzoefu katika ngazi ya klabu na kimataifa na ana sifa zote ambazo zinahitajika kufana katika Ligi ya Premia," mkurugenzi wa kiufundi wa Chelsea Michael Emenalo alisema. "Ni mchezaji ambaye uwezo wake umethibitishwa." Rudiger atavalia jezi nambari mbili ambayo iliachwa wazi baada ya Branislav Ivanovic k

Harnaam Kaur ni mwanamke anayefuga ndevu

Image
  Harnaam Kaur ni mwanamke anayefuga ndevu  "Nilianza kufuga ndevu nilipokuwa na umri wa miaka 16. Nilikuwa na nywele zilizojaa usoni tangu nibalehe, ikafikia wakati ambapo nilifikiri iwapo nywele hizo zingeendelea kuota katika uso wangu nitazikubali na kuziruhusu kumea. Nilichokozwa shuleni kutokana na nywele zilizokuwa zikimea usoni. Wazazi wangu walikuwa na wasiwasi na hali yangu ya afya kwa jumla. Uchunguzi wa hospitali ulibaini kwamba nina homoni nyingi za kiume ikilinganishwa na zile za kike swala linalosababisha kumea kwa ndevu hizo. Mwanamke avunja rekodi ya ndevu Shule ya watu waliobadili jinsia yafunguliwa India Zsa Zsa Gabor, mwigizaji aliyeolewa mara tisa Nilijaribu kila njia kuzinyoa nywele zilizokuwa zikimea usoni mwangu. Nilijaribu kubadili rangi ya ngozi, kunyoa, kutumia mafuta ya kuondoa nywele bila mafanikio. Nilinyoa kila siku. Lakini nywele hizo ziliendelea kuwa nyeusi na ndefu zaidi. Nilikuwa na marafiki walionitunza walionijali san

Wayne Rooney: Ninasubiri kwa hamu sana kwenda Tanzania

Image
Nyota wa soka wa England Wayne Rooney, ambaye amekamilisha uhamisho wake kutoka Manchester United na kurejea Everton amesema anasubiri kwa hamu sana kuzuru Tanzania. "Naisubiri sana kwa hamu na ghamu (safari ya kwenda Tanzania) - inafaa kuwa safari nzuri," aliambia runinga ya evertontv. "Itakuwa nzuri sana na natumai kwamba nitaweza kuingia uwanjani na kucheza. "Huwa vizuri sana unaposafiri na timu. Ni vizuri kuwa hotelini na wachezaji, kujumuika nao na kuwafahamu zaidi. "Sijawahi kwenda Tanzania, na kwa hivyo nasubiri sana kwenda huko." Rooney atakuwa kwenye kikosi cha Everton kitakachocheza mechi ya kujiandaa kwa msimu ujao katika taifa hilo la Afrika Mashariki. Mkenya ashinda dola 2m shindano la bahati nasibu Klabu ya Everton kucheza nchini Tanzania Amesema ziara hiyo itampa fursa mwafaka ya kufahamiana na wachezaji wenzake wapya. says Everton's pre-season trip to Tanzania provides the perfect opportunity for him to get to know his n

Mishahara ya rais na wabunge yapunguzwa

Image
  Tume ya mishahara na marupurupu ya watumishi wa umma nchini Kenya imetangaza kupunguzwa kwa mishahara ya maafisa wakuu wakiwemo rais na wabunge. Mwenyekiti wa tume hiyo Bi Sarah Serem ametoa mpangilio mpya wa malipo ambao anasema utaokoa jumla ya Sh8 bilioni (dola 80 milioni za Marekani) kila mwaka na kupunguza jumla ya mishahara inayolipwa watumishi wa umma kwa asilimia 35 . Tume hiyo imependekeza kufutiliwa mbali kwa marupurupu ya kipimo cha usafiri wa magari kwa magavana na wabunge na badala yake hilo litakuwa likifidiwa na mfumo mpya wa marupurupu kwa kuzingatia kanda. Rais sasa atakuwa akilipwa Sh1.4 milioni (dola 14,000) kila mwezi badala ya Sh1.65 milioni (dola 16,500), naye naibu wake awe akilipwa Sh1.2 milioni (dola 12,000). Mawaziri watakuwa wakilipwa Sh924,000 (dola 9,200), Spika wa Bunge Sh1.1 milioni (dola 11,000) nao magavana wa kaunti Sh924,000 (dola 9,240). Mabadiliko hayo yataanza kutekelezwa tarehe 8 Agosti, 2017. Bi Serem amesema maafisa wa