Mtulia amkana Salum Mwalimu hadharani

Aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Kinondoni Maulid Mtulia amemkana mgombea ubunge wa CHADEMA, Salum Mwalimu kwamba hakuwahi kumpigania kwa namna yoyote wakati wa uchaguzi mkuu 2015 alipokuwa mgombea wa jimbo hilo kupitia CUF chini ya mwamvuli wa UKAWA.
 
Leo asubuhi kupitia kipindi cha East Africa Breakfast ndani ya EA radio Mtulia ambaye ni mgombea wa Ubunge wa Knondoni kupitia CCM  ameyasema hayo wakati akijibu swali la Salum Mwalimu ambaye ni mshindani wake kwa sasa katika uchaguzi huo kupitia CHADEMA, baada ya kumuuliza anajisikia vipi baada ya kuwasaliti wana kinondoni ambao,  baadhi yao walipoteza maisha yao  wengine kubaki vilema na hata wajawazito kupoteza mimba zao wakati wakishinikiza mgombea wao (Mtulia) atangaziwe ushindi 2015.
Mtulia amesema kwamba, Mwalimu kumuambia kwamba alimpigania si kweli  kwani wakati wakati wa uchaguzi 2015, Mwalimu alikuwa anampigania mgombea mwingine wa jimbo la kikwajuni hivyo ana uhakika kwamba Mwalimu, (ambaye wakati huo alikuwa Katibu Mkuu) hakumpigania na kama yeye ndiye aliyempigania basi angejipigania mwenyewe ili ashinde.
Aidha Mtulia ameongeza kwamba "Mimi  nimejiuzulu kwa sababu ya maslahi ya wana kinondoni. Yale niliyokusudia kuyafanya kama tungekuwa na serikali ya UKAWA ambayo kiongozi wangu alikuwa akiipigania tungeyafanya, kwa kuikosa serikali ya UKAWA tukabaki ukiwa. Wananchi wangu waelewe kwamba Mbunge wao nimehamia huku kwa ajili ya maslahi yao kuliko kuendela kupokea mishahara na posho tu.
Mtulia mwaka 2015 alishinda uchaguzi wa jimbo la Kinondoni kwa tiketi ya CUF ambayo ilikuwa chini ya mwamvuli wa UKAWA unaounganisha vyama vinne vikiwepo, CHADEMA, CUF, NCCR na NLD.

Comments

Popular posts from this blog

DOWNLOAD NA USIKILIZE NYIMBO ZA KWARESIMA